Ecclesiastes 7:3-6


3 aHuzuni ni afadhali kuliko kicheko,
kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.

4 bMoyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba,
lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.

5 cAfadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima,
kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.

6 dKama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria,
ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu.
Hili nalo pia ni ubatili.

Copyright information for SwhKC